Tuesday, May 23, 2017
Sunday, May 14, 2017
Monday, May 8, 2017
Sportpesa yahamia kwa Simba na Yanga
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEidzMwus1Lzlze80nxBcXa65i3SqjAhB8MCHvfSdxbjyOdR_I19uVInOH_07AR0Kj8C-yFY66tHCr94-hXI_5l0pShsRI7t9MkJRIYinRsMbxG8hISWbcgwc71JyznGy9GVRk_SK-KD/s640/gor_thikawin.jpg)
THAMANI ya Ligi Kuu ya Kenya maarufu kama Kenya Premier League
imekuwa ikipanda kwa kasi kubwa na kuanza kurejesha heshima ya soka la
Kenya.
Kabla, soka la Kenya lilionekana limepoteza mvuto kabisa na kwa zaidi ya misimu nane limekuwa likisuasua na kuandamwa na migogoro ya kila aina.
Shirikisho la Soka la Kenya (FKF), chini ya mkongwe Sam Nyamweya lilionekana kupoteza mwelekeo na mambo yakazidi kuwa magumu.
Ilifikia wakati kukawa na ligi mbili ndani ya nchi moja. Ligi moja ilisimamiwa na FKF na nyingine bodi ya ligi.
Mwisho wa msimu, kukawa na bingwa wawili, washindi wa pili wawili halikadhalika watatu na wengineo. Hii ilikuwa ni sehemu ya kuonyesha kwamba soka la Kenya limekosa mwelekeo kabisa.
Kabla, soka la Kenya lilionekana limepoteza mvuto kabisa na kwa zaidi ya misimu nane limekuwa likisuasua na kuandamwa na migogoro ya kila aina.
Shirikisho la Soka la Kenya (FKF), chini ya mkongwe Sam Nyamweya lilionekana kupoteza mwelekeo na mambo yakazidi kuwa magumu.
Ilifikia wakati kukawa na ligi mbili ndani ya nchi moja. Ligi moja ilisimamiwa na FKF na nyingine bodi ya ligi.
Mwisho wa msimu, kukawa na bingwa wawili, washindi wa pili wawili halikadhalika watatu na wengineo. Hii ilikuwa ni sehemu ya kuonyesha kwamba soka la Kenya limekosa mwelekeo kabisa.
Miaka minne iliyopita wakati Nyamweya anakaribia kuondoka, timu ya taifa
ya Kenya “Harambee Stars” chini ya Kocha Adel Amrouche, ilifanikiwa
kutwaa ubingwa wa Kombe la Chalenji lililofanyika nchini humo.
Wengi walishangazwa na sifa nyingi zikaenda kwa kocha Amrouche raia wa
Ubelgiji mwenye asili ya Algeria. Kwamba ana uwezo wa kufanya katika
mazingira magumu kama alivyokuwa akiifundisha Burundi.
Uchaguzi uliofuata, Nyamweya aliangushwa na Nick Mwendwa, akiwa ni rais
kijana kushika nafasi hiyo. Wengi waliingiwa hofu angeweza vipi
kuendesha mambo naye alikubaliana na hali haikuwa nzuri.
Mwaka wa kwanza, hali ilionekana kuzidi kuwa ngumu na ule usemi kwamba angekwama ukazidi kuchukua nafasi.
Lakini wakati ikionekana na Mwendwa alikuwa ameshindwa, ghafla mambo yalibadilika na kuanza kwenda kwa kasi kubwa.
Wengi wakaonekana kushangazwa kwa kuwa Kenya ilikuwa kati ya timu
zilizokuwa chini ya kiwango cha 130 katika viwango vya soka vya Fifa.
Hawakuwa tena na tofauti na Tanzania ambao angalau walikuwa na nafuu.
Utaona ule mlolongo wa wachezaji wengi wa Kenya na hata Uganda
kukimbilia Tanzania ulizidi kuongezeka kwa kuwa hata zile timu kama
Sofapaka zilizokuwa zikilipa vizuri zilidorora na wakongwe Gor Mahia na
AFC Leopards walikuwa wameyumba na kuonekana hawana nafasi kwani kila
walipoinuka walianza kuyumba tena.
Mwendwa akaonekana ni shujaa, lakini ukweli ni udhamini mnono ambao
walianza kuufanya kampuni ya masuala ya michezo ya kubahatisha ya
SportPesa.
SportPesa walidhamini timu zote kongwe mbili za Gor Mahia na AFC Leopard
na kawaida wao ndiyo chachu ya ushindani. Pia wakadhamini timu nyingine
na Nakuru All Stars.
Kama hiyo haitoshi, kampuni hiyo ikaingiza udhamini mnono katika Ligi
Kuu Kenya na kufanya kuwe na ushindani zaidi kwa kuwa fedha hizo
zinaingia kwenye mifuko ya timu zote 18 zinazoshiriki ligi hiyo.
Ukiangalia thamani ya ligi ya Kenya imepanda, ushindani umerudi na
hamasa hata ya mashabiki kwenda viwanjani imerudi kwa kasi kubwa na sasa
ni kati ya ligi zilizo juu katika Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.
Taarifa zimekuwa zikieleza SportPesa tayari wako nchini na wamenuia
kuzidhamini Yanga na Simba ambazo ni timu zenye mashabiki zaidi katika
ukanda huu.
Inawezekana siku moja wakaingia kwenye ligi lakini kampuni hiyo kama itatumika vizuri basi inaweza kurejesha hamasa tena.
Huenda tuaona kawaida lakini mfano mzuri, Simba kwa msimu mzima wa 2016-17 imecheza kwa hasara kama tulivyowahi kuandika makala.
Kwamba hawana mdhamini na vifua vyao ni mali, lakini hakukuwa na
aliyeona thamani yao baada ya kujiondoa kwa Kampuni ya Bia Tanzania
(TBL).
Shukrani kwa TBL kwa kuwa waliweza kujali angalau kwa misimu kadhaa.
Lakini kama SportPesa basi ndiyo wakati mwingine wa kurejesha heshima ya
soka nchini.
Hakuna unapoweza kukwepa fedha katika maendeleo ya soka. Vizuri pia kufanya kazi na watu waliojifunza kupitia hatua mbalimbali.
Mfano SportPesa wanadhamini timu ya Ligi Kuu England (EPL), Hull City.
Unapozungumzia udhamini wanajua nini cha kufanya kusaidia zaidi.
Kawaida wadhamini walioendelea hupenda mafanikio kwa wale
wanaowadhamini. Hii ni nafasi kwa Yanga na Simba kubadili mambo na hasa
kama wataingia udhamini, basi fedha watakazozipata ziwe kwa ajili ya
maendeleo na si mifuko ya wahusika.
SportPesa ni sehemu wa wadhamini wa klabu maarufu ya Arsenal ya England.
Hivyo wanajua kitu kinachoweza kuwasaidia Yanga na Simba lakini soka la
Tanzania.
Kikubwa ambacho SportPesa wamekuwa wakikifanya ni kurudisha kiasi cha
fedha kwa jamii kama udhamini. Wameweza kuzirudisha Gor Mahia na AFC
Leopards katika ramani ya soka zikiwa na nguvu.
Simba na Yanga hazikuwa zimekufa lakini mwendo wao ulikuwa unaashiria
“kifo”. Sasa ndiyo wakati mwafaka wa kutumia vizuri udhamini huo
unaelezwa kuwa utakuwa mkubwa zaidi kuliko waliowahi kupata hapo awali.
Benki Kuu ya Tanzania (BoT) yaifutia leseni benki ya FBME
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiIC8lKgruOHfxf9NnVQ3hvGV8CVMdXM3PsPbYFllyjVF3Xw5MW9b1aqRc4NdLlTnZHkw7ReGbu3AdnmqSSHh7lKP_ZKpgo3nVCPJRmasGTDl-c_f8O75NKIebivmXRhL38FVu-OHT35GvR/s640/1.jpg)
Benki
Kuu ya Tanzania (BoT) imeifutia leseni ya biashara Benki ya FBME na
kuteua Bodi ya Bima ya Amana kuwa mfilisi kuanzia leo.
Taarifa
iliyotolewa na BoT inawataka wenye amana, wadai na wadaiwa kuwa
wavumilivu wakati mfilisi akiandaa utaratibu wa kushughulikia stahiki
zao.
“Mfilisi
kwa wakati muafaka atawafahamisha wenye amana, wadai na wadaiwa
utaratibu wa malipo ya madai, ulipaji wa madeni na taratibu nyingine
zinazohitajika kwa mujibu wa sheria,” inasomeka sehemu ya taarifa hiyo.
Uamuzi huu wa BoT umetolewa baada ya hukumu ya kesi ya utakatishaji fedha iliyokuwa ikiikabili benki hiyo kutolewa.
Itakumbukwa,
mwaka 2014, Mtandao wa Kudhibiti Uhalifu wa Masuala ya Fedha (FinCEN)
wa Marekani uliitaja FBME kuwa taasisi inayojihusisha na utakatishaji
fedha hivyo kuizuia kutoa huduma nchini humo.
Machi
mwaka jana, msimamo wa FinCEN uliendelea kuwa huohuo hata Aprili 14,
mahakama moja jijini Washington, DC ilitoa hukumu inayoupendelea mtandao
huo. Nakala za hukumu hiyo imetumwa kwa BoT na Benki Kuu ya Cuprus kwa
hatua zaidi.
Baada
ya hukumu hiyo iliyosomwa na Jaji Christopher Cooper, benki hiyo yenye
makao makuu yake nchini na matawi huko Cyprus italazimika kurudisha Dola
2.6 bilioni za Marekani ambazo ni amana za wateja wake ndani ya siku
90.
MUHIMU:Hivi Ndiyo Earphone Zilivyo Hatari Kwenye Masikio
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi57-11EnGEVEiZ2mL5O60eNhGv83TTXh6YFWRh0WsaD8kl5TUrUpGAOhNiv_KdOT9F87ZIB-WeuHrIpwSgv8hwk0HKTKcQoTE1wj38avThg0-GNbmpP7XHAmcdPDqbL6v5zT1yTwGd3cs/s640/2.jpg)
Kundi
kubwa la watu watumiaji wa spika ndogo za masikioni (earphone), hasa
wanahabari na wanafunzi, wako hatarini kupata magonjwa mbalimbali
yanayotokana na vijidudu vinavyoambukiza, uchunguzi umebaini.
Uchunguzi
huo umebaini kuwa ni jambo lililozoeleka kwa wanahabari wanapokuwa
vyumba vya habari au maofisini, kuazimana spika hizo bila kuchukua
tahadhari za kiafya.
Mbali
na kundi hilo, kundi kubwa la vijana wadogo, hasa wanafunzi, pia liko
katika hatari ya kupata maambukizo ya magonjwa ya masikio kutokana na
mazoea hayo ya kuchangia matumizi ya spika hizo.
Watu
mbalimbali waliohojiwa, wameelezea kutoelewa athari zinazoweza
kusabishwa na kuchangia earphone ambazo huweza kubeba magonjwa ya ngozi
na yale ya masikio kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine.
Dk
Kareem Segumba alisema uchangiaji wa ‘earphone’ si jambo zuri kwa kuwa
husababisha maambukizi ya magonjwa mbalimbali kutoka kwa mtu mmoja
aliyeathirika kwenda kwa mwingine.
“Kitaalamu tunasema anapata contagious (maambukizi) ya magonjwa ya sikio toka kwa mgonjwa. Magonjwa haya ni pamoja na fungus ya masikio,” alisema Dk Kareem.
Dk
Kareem, ambaye amehudumu katika hospitali mbalimbali nchini, alitaja
magonjwa mengine kuwa ni maambukizi ya sikio sehemu ya mzunguko na
maambukizi kwenye ngoma ya sikio.
“Mara
nyingi mtu anayeumwa fangasi ya sikio au kutokwa na majimaji kidogo
kabla ya kugeuka usaha huwa hawajitambui. Wengi wanajua baada ya kuona
usaha,” alisema.
“Si
desturi nzuri kuchangia earphone na mtu yeyote kwa kuwa madhara yake ni
makubwa na hasa ukizingatia masikio yako karibu sana na ubongo na
huenda ukapata maambukizi kupitia mishipa.
“Mishipa
ya damu inapeleka vijidudu vya ugonjwa kwenye ubongo na hatimaye
kutokea athari nyingine kama uziwi, kupoteza nguvu ya kuona na matatizo
kwenye uti wa mgongo.”
Mpigapicha
wa kituo cha televisheni cha ITV mkoani Kilimanjaro, Robert Minja
alikiri watu wengi hususan wanahabari wamekuwa na tabia ya kuchangia
earphone, kwa vile hawajui madhara.
“Hilo
la ku- share earphone (kuchangia) lipo sana na inavyoonekana watu wengi
hawajui madhara yake. Tunaona ni mambo ya kawaida lakini kiukweli hii
tabia ina madhara ya kiafya,” alisema.
Maulid
Rashid, ambaye ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Stefano
Moshi (Smmuco) alisema tatizo la kuchangia vifaa hivyo ni kubwa chuoni
hapo.
“Ni
kweli wanafunzi wengi wanachangia hizo earphone. Nafikiri wanaofanya
hivyo hawana uelewa kuwa kuna madhara. Yaani hili ni tatizo kubwa si kwa
wanafunzi tu hata watu wa kawaida,” alisema.
Subscribe to:
Posts (Atom)